![]() | |
Cheka akiwa chini ya Ulinzi Mkali Mahakamani |
Bondia Francis Bonifas Cheka amepandishwa kizimbani leo katika mahakamani ya hakimu mkazi mfawidhi mkoa wa Morogoro kwa mara ya kwanza na kusomewa shitaka la shambulio la kumpiga na kumjeruhi aliyekuwa meneja wa baa yake.
Akisoma
mashitaka mbele ya hakimu wa mahakama ya mkoa wa Morogoro Saidi Msuya mwendesha
mashitaka Aminata Mazengo amesema julai 02 mwaka huu Cheka bila halali na huku
akijua ni kosa kisheria kifungu namba 241
cha makosa ya jinai alimpiga ngumi Bahati Kabanda kichwani na tumboni na
kumsabishia maumivu makali.
![]() | |
Meneja wa Baa ya Vijana Social hall Bahati Kabanda iliyechezea kichapo kutoka kwa Bondia Francis Cheka |
Cheka ambaye ni Bondia wa ngumi za kulipwa namba moja nchini na anayeshikilia mkanda wa WBF, inadaiwa kumpiga meneja wake wa baa baada ya meneja huyo kushindwa kumkabidhi hela inayopatika katika baa hiyo hali iliyopelekea bondia huyo kumshushia kipigo.
![]() | |||||
Waandishi wa Habari nao hawakuwa nyuma kufuatilia tukio hilo |
Mtuhumiwa
katika kesi hiyo amekana mashtaka na Kesi
hiyo imehairishwa na inatarajia kusikilizwa tena julai 23 huku Cheka
akiachiwa kwa dhamana baada ya Mahakama kutoa masharti ya dhamana, ikimtaka
Mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili na kila mmoja kuweka dhamana ya maandishi ya
shilingi milioni moja ambayo ilitimizwa.
No comments:
Post a Comment