![]() |
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Ulrich Mtei akizungumza na Waandishi wa Habari ambao hawako Pichani |
Watu watatu wamefariki Dunia na wengine wawili kujikuta katika hali mbaya, mara baada ya kudaiwa kula mihogo inayodhaniwa kuwa na sumu, katika kijiji cha Kauzeni kilichopo kata ya Mzinga Manispaa ya Morogoro huku kati yao, wawili wakiwa ni ndugu wa familia moja.
Tukio hilo limetokea wakati watu hao wakiwa wanajiandaa kuanza kutengeza matofali, na ndipo walichemsha mihogo hiyo na kula, na baada ya muda mfupi hali zao zilibadilika na kukimbizwa katika hospitali ya Jeshi ya Mzinga, hata hivyo walihamishiwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro baada ya hali zao kuwa mbaya zaidi..
Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Ulrich Mtei, amesema jeshi la Polisi Mkoani humo linaendelea na uchunguzi, kujua sumu hiyo iliweka kwenye chakula hicho au ilikuwa kwenye mihogo, huku akisema kati ya marehemu waliofariki dunia, wawili ni ndugu wa familia moja ambao ni mapacha waliojulikana kwa majina ya Omary Issa Mohamed na Hamis Issa Mohamedi huku mwingine akijulikana kwa jina la Wakusizi.
.
![]() |
Mmojawapo Aliyenusurika katika tukio hilo Anaitwa Joshua Msiani
|
Kamanda Mtei amesema miili ya Marehemu watatu waliofariki kutokana na kula mihogo hiyo yenye sumu, imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospital ya rufaa ya mkoa wa Morogoro kusubili taratibu za mazishi kutoka kwa ndugu wa marehemu.
Hatua nyingine mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Jackson John ambaye inasadikiwa ni mgonjwa wa akili, amemuua ndugu yake wa damu (Mdogo wake) aitwaye Raymond Meckioli (9) ambaye ni mwanafunzi wa darasa wa Pili, katika shule ya Msingi Kikeo, wilayani Mvomero, kwa kumchoma na mkuki tumboni, kisha na yeye kujiua kwa kutumia mkuki huo huo, kwa kujichoma sehemu ya ubavuni.
MWISHO:
No comments:
Post a Comment