Tuesday, July 19, 2016

KIWANDA CHA NGUO CHA 21 CENTURY KILICHOPO MOROGORO CHATEKETEA NA MOTO


Kiwanda cha nguo cha 21 Century kilichopo Kihonda Maghorofani mkoani Morogoro Kimeteketea na moto asubuhi ya leo ya uliosababishwa na hitilafu ya umeme ambapo wafanyakazi waliokuwa zamu wanasema umeme huo umeanzia katika mashine namba moja na kusambaa katika nguo na Pamba.




Kiwanda hicho chenye wafanyakazi zaidi ya 1600 kililazimika kusitisha shughuli zake za uzalishaji kwa kuwaruhusu wafanyakazi wake kurudi majumbani kupumzika huku taasisi husika zikiendelea na jukumu la kuzima moto kwa kusaidiana na kikundi maalumu kilicho kiwandani hapo.

Katika Ajali hiyo askari mmoja wa  Jeshi la zimamoto na Uokoaji amedondokewa na kitu chenye incha kali kichwani wakati akiwa katika harakato za uokoaji na kukimbizwa hospitali ya rufua ya mkoa kwa ajili ya matibabu zaidi.


Akizungumza na Mtandao huu Meneja uzalishaji wa kiwanda hicho Clement Munisi amesema idadi kubwa ya mashine ndizo zilizoteketea katika ajali hiyo ya moto huku moto huo ukianzia katika plate mashine baada ya kuanza kutokea cheche zilizopelekea moto huo kutokea na kuanza kusambaa sehemu mbalimbali za kiwanda hicho.

Mpaka mtandao huu unatoka eneo la tukio harakati za kuendelea kuuzima moto huo ulikuwa bado unaendelea kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho pamoja na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.



Marobota ya nguo pamoja na Pamba ndizo zilizoteketea zaidi katika ajali hiyo ya moto, huku thamani ya vifaa vyote vilivyoteketea na moto huo bado havijabainishwa.

Hata hivyo wafanyakazi wa kiwanda hicho wameuambia mtandao huu kuwa mashine hiyo namba moja ambayo ndiyo chanzo cha moto huo imekuwa ikitoa cheche mara kwa mara wakati wa uzalishaji.


MWISHO:

No comments:

Post a Comment