Wednesday, August 24, 2016

ALIYEWAHI KUWA MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO ABDUL MTEKETA ATOA MSAADA WA MAGODORO 200 WILAYANI KILOMBERO


Na,Mohamed Ferooz
IFARAKARA/MOROGORO

Ukosefu wa gari la wagonjwa, uhaba wa watumishi na vifaa tiba ni changamoto ambazo zimeendelea kuiandama hospital ya Wilaya ya kilombero mkoani Morogoro, hatua iliyopelekea kushindwa kutoa huduma stahiki kwa wananchi wanaoishi wilayani humo. 




Kutokana na ongezeko la kasi la idadi ya watu Wilayani humo, imeleezwa kuna kila haja  kuboresha huduma hizo mhuhimu, ili kukidhi mahitaji ya huduma za kimatibabu, zinazohitajika wilayani humo.

Akizungumza na mtandao huu wakati akipokea msaada wa magodoro kutoka kwa mbunge mstaafu wa jimbo hilo Abdul Mteketa, Mganga mkuu wa kituo hicho cha Kibaoni Peter Mlenge amesema kutokana na hospitali hiyo kutarajiwa kuwa hospitali ya halmashauri ya mji wa ifakara inabidi wadau na serikali kuongeza jitihada za kuiborsha hospitali hiyo ambayo hali yake sio nzuri kimuonekano pamoja na huduma kutokana na ukosefu wa wataalamu na pamoja na vifaa. .

 
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kilombero Abdul Mteketa akizungumza na waandishi wa Habari ambao hawako kichwani.
Aliyewahi kuwa mbunge katika jimbo hilo la Kilombero kupitia chama cha mapinduzi CCM abdul Mteketa anahitikia wito huo na kumua kutoa msaada wa magodoro 50 katika hospitali hiyo huku magodoro mengine 150 akitoa kwa watu kwa wazee, wakimama na watu wasiojiweza wilayni humo..



MWISHO:




No comments:

Post a Comment