Tuesday, August 23, 2016

KATIBU WA CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU MANISPAA YA MOROGORO MMFA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA RUSHWA YA CHAKULA WAKATI WA UCHAGUZI WA CHAMA HICHO

NA, Happynes James
Morogoro
 

Katibu wa chama cha mpira wa miguu manispaa ya Morogoro (MMFA )  Kafale Maharagande amefikishwa mahakamani na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru mkoani humo kwa tuhuma za kutoa rushwa ya chakula chenye thamani ya shilingi milioni moja na laki tano (1,500,000)  kwa wajumbe wa chama hicho hili wamchague wakati wa uchaguzi.  

Katibu wa MMFA Kafale Maharagande akiwa Mahakamani


Akisomewa mashtaka hayo na mwendesha mashtaka wa Tukukuru mkoani Morogoro Cleonce Cleophace mbele ya hakimu mkazi Ivan Msacky, mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kutenda kosa hilo julai 24 mwaka huu wakati wa uchaguzi wa chama hicho ambapo alichaguliwa tena kuwa katibu wa chama hicho cha mpira wa miguu..

Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU mkoani Morogoro Cleonce Cleophace akinena jambo na mmiliki wa Blog Hii.

Ikiwa umepita mwezi  mmoja na siku moja tangu kufanyika kwa uchaguzi wa MMFA, ambao ulimtangaza Kafare Maharagande kuwa katibu mkuu wa chama hicho,   mpinzani wake Jofrey Mwatesa  hakuridhishwa na matokeo hayo, hatua iliyopelekea kuandika barua ya kukata rufaa kwa kamati ya uchaguzi na nakala kupeleka TAKUKURU kupinga matokea hayo kwa madai ya katibu huyo kutoa rushwa ya chakula kwa wajumbe wa chama  hicho.



Kukiwa na hali ya bado sintofahamu kwa kamati ya uchaguzi iliyosimamia uchaguzi huo kuhusu sakata hilo, Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani humo, wanamfikisha katibu huyo mahakamani tayari kujibu tuhuma  hizo zinazomkabili.

Hata hivyo mtuhumiwa huyo amekana kutenda makosa  hayo licha ya upande wa TAKUKURU kuikikishia mahakama kuwa ushahidi wa tuhuma hizo ushakamilika.

Kesi hiyo inatarajiwa kuendelea tena Septemba  mosi mwaka huu huku mtuhimiwa huyo akiwa nje kwa dhamana.

MWISHO:




No comments:

Post a Comment