![]() | |
| Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya siasa |
Viongozi wa
vyama vya siasa nchini wameiomba serikali kupitia upya sheria na kanuni za
uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Octoba mwaka huu.
Hayo
yamebainishwa mkoani morogoro na mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahimu Lipumba na Naibu katibu wa
Chadema John Mnyika katika mkutano wa
viongozi wa vyama vya siasa ngazi ya taifa ya kujadili maoni ya wadau
mbalimbali ya kuboresha kanuni za
uchaguzi wa viongozi wa mamlaka za serikali za mitaa huku wakisema kanuni hizo
bado haziko sahihi kwani hazikufanyiwa mabadiliko tangu mwaka 2009.
![]() | |
| Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Pro Ibrahim Lipumba |
![]() |
| Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini, pia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent Kalogeresi |
Viongozi hao
pia wamesema serikali hakuzingatia maoni ya wadau kuhusu maboresho ya kanuni za uchaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa
tangu mwaka 2009 mpaka sasa, hali inayosababisha uchaguzi huo kuwa sio wa haki.
Kwa upande
wake waziri wa Nchi ofisi ya waziri mkuu, amesema kuwa baadhi ya mapendekezo
katika uchaguzi wa seriakali za mitaa wa 2009 yamefanyiwa kazi Kazi na kweka
katika kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa, huku akiwaasa viongozi wa vyama
vya siasa kuangalia jinsi ya kuweza kukabiliana na changamoto zilizojitokeza
kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2009
Pia amewatoa
hofu viongozi wa vyama vya siasa kuhusu kuwa na imani na wakurugenzi wa
halmashauri wa manispaa zote nchini, kwani wanateuliwa kutokana na uwezo
waol binafsi bila kujali itikadi zao za vyama.
Mkutano huo
wa viongozi wa vyama vya siasa ngazi ya taifa
utadumu kwa muda siku mbili mkoani Mkoani Morogoro ukiwa na malengo ya kuboresha kanuni za
uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka
2014.






No comments:
Post a Comment