Ofisi ya Rais Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeigiza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro
kuunda kamati ya Uchunguzi ambayo itajihusisha kuchunguza tuhuma za matumizi
mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo ambazo zimeelekezwa kwa mkurungezi wa
Halmashauri ya Gairo mkoani humo Kibwana
Magota.
Imeelezwa kuwa tume
hiyo itafanya kazi hiyo ndani ya siku saba na itamuhoji mkurungezi huyo, baadhi
ya wakuu wa idara pamoja na madiwani, na baada ya kukamilika kwa uchunguzi huo,
taarifa hiyo itafikishikishwa kwa waziri wa TAMISEMI kwa ajili ya
kuchukua maamuzi.
Katika kikao maalumu
cha Baraza la Madiwani cha Mei 7 mwaka huu, kiliadhimia kutokuwa na imani na
mkurungezi wa Halmashauri hiyo, huku katika kikao cha kamati ya fedha cha Mei
13, wajumbe wa kamati hiyo, nao , walisusia kikao hicho mpaka hapo tuhuma
zinazoelekezwa kwa mkurungezi huyo zitakapofanyiwa kazi.
Hatimaye Ofisi ya Rais
Tawala za mikoa na Serikali za mitaa imeweza kuingilia kati mvutano huo, baada
ya kuitaka Serikali ya mkoa kuunda kamati ya uchunguzi, kwa wale ambao tuhuma
hizo zinaelekezwa kwao, na taarifa hizo zifikishwe kwa waziri ndani ya
siku ya saba tayari kwa kuwachukulia hatua hayo yamebainishwa na katibu tawala
wa mkoa wa morogoro Dr John Ndunguru pamoja na mkuu wa mkoa huo Dr Kebwe
Stephen.
Huku mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr Stephen Kebwe akiwataka madiwani hao, kukubali kushiriki katika vikao
vitakavyoandaliwa na Halmshauri hiyo, wakati suala lao la tuhuma kwa
mkuruigenzi wa halmashauri hiyo likifanyiwa.
Madiwani wa
Halmashauri ya Gairo waliadhimia kutofanya kazi na mkurungezi wa halamshauri
hiyo kwa madai ya kutoridhishwa na utendaji wake hasa katika kupanga na
kufatilia miradi ya maendeleo na kutaka madai yao kufikishwa TAMISEMI.
No comments:
Post a Comment