ZUKU
TANGAZO

KIBUNGO JUU

Monday, February 26, 2018
BREAKING NEWS: MBUNGE WA MBEYA MJINI JOSEPH MBILINYI 'SUGU' AMEHUKUMIWA KWENDA JELA MIEZI MITANO
Tuesday, January 16, 2018
FEDHA BANDIA ZENYE THAMANI YA SHILINGI MIL 40.6 ZAKAMATWA MKOANI MOROGORO
Morogoro
Na, OmaryHussein
Watu watano wanashikiliwa na Polisi mkoani Morogoro, kwa makosa
tofauti yakiwemo ya watu wawili kukutwa na pesa bandia zenye thamani ya
zaidi ya shilingi Milion 40.6 na mabunda 22 ya karatasi
zinazotumika kutengeneza noti hizo, huku wengine wawili wakikutwa
na vipande 4 vya pembe za Ndovu.
Monday, January 15, 2018
WATU 11 WAMEFARIKI DUNIA NA WENGINE SITA KUJERUHIWA BAADA YA GARI AINA YA HIECE KUGONGANA NA MALORI MATATU
KAGERA,
Na, Mariam Emily
Watu 11 wamefariki dunia na wengine sita kujeruhiwa kutokana na ajali ya gari aina ya hiece kugongana na malori matatu katika kijiji cha Mubigera kata ya Nyantakara wilaya ya biharamulo mkoani kagera wakati wakisafiri kutoka wilaya ya kibondo kuelekea kahama mkoani Shinyanga.

Sunday, January 14, 2018
BOMOA BOMOA MWANZA YAWALIZA WAFANYABIASHARA WA SAMAKI NA DAGAA

Kampuni hodhi ya rasilimali za reli nchini (Rahco) imeanza utekelezaji wa kubomoa nyumba zote zilizojengwa ndani ya njia ya reli katika mkoa wa Mwanza huku zaidi ya wafanyabiashara 200 wa samaki na dagaa jijini humo wakikosa sehemu ya kwenda kufanyia biashara zao baada ya kubomolewa vibanda vyao.
Thursday, December 28, 2017
MAUTI ILIYOZIKWA ZAIDI YA MWEZI MMOJA ULIOPITA YAFUKULIWA KWA LENGO LA KUCHUNGUZWA
GAIRO,MOROGORO
NA, OMARY HUSSEIN
Huzuni
na simanzi zimetawala kwa zaidi ya masaa nne kwa wakazi wa kijiji cha Kilimani
kata ya Msingisi wilaya ya Gairo mkoani Morogoro baada ya familia ya watoto
wanne wakiongozwa na mama yao mzazi kufika kijijini hapo na kufukua kaburi
alipozikwa baba yao aliyezikwa miezi miwili iliyopita, wakidai kuwa na mashaka na
kifo chake ikiwa ni sehemu moja wapo ya kutekeleza agizo la mahakama ya hakimu
Mkazi mkoa wa Morogoro.
UJENZI WA GHOROFA UMEKULA KERO KWA UWANJA WA NDEGE WA NJOMBE
NJOMBE
Licha ya naibu waziri wa Ujenzi ,Mawasiliano na Uchukuzi Dkt John Elias Kwandikwa kutoa agizo la kusitisha ujenzi wa jengo refu la Ghorofa Mbele ya uwanja wa Ndege wa mkoa wa Njombe ili kuacha wazi eneo hilo la ndege kupaa, agizo hilo limeonekana kupuziwa kwani ujenzi huo umeendelea kama kawaida.
Subscribe to:
Posts (Atom)