GAIRO,MOROGORO
NA, OMARY HUSSEIN
Huzuni
na simanzi zimetawala kwa zaidi ya masaa nne kwa wakazi wa kijiji cha Kilimani
kata ya Msingisi wilaya ya Gairo mkoani Morogoro baada ya familia ya watoto
wanne wakiongozwa na mama yao mzazi kufika kijijini hapo na kufukua kaburi
alipozikwa baba yao aliyezikwa miezi miwili iliyopita, wakidai kuwa na mashaka na
kifo chake ikiwa ni sehemu moja wapo ya kutekeleza agizo la mahakama ya hakimu
Mkazi mkoa wa Morogoro.
Wanafamilia hao walifika kijijini hapo wakiwa na ulinzi wa polisi kwa
ajili ya kusimamia kufukuliwa kwa kaburi hilo na watoto hao kupata nafasi ya
kuhakikisha kama mwili uliozikwa ni baba yao mzazi au siyo pamoja na kufanyiwa
uchunguzi kubaini sababu zilizopelekea kifo chake huku wakisema kilicho wasukuma kufika mahakamani
ni kutokuwepo maelewano mazuri baina ya ndugu wa upande wa baba yao kutokana na marehemu huyo kufariki na kuzikwa
bila kupewa taarifa yoyote walisema watoto wa Marehemu Merina na Yared Stanford.
![]() |
Baadhi ya watoto wa Marehemu wakitafakari baada ya kuona mwlili wa marehemu baba yao |
Kwa mujibu wa Mke wa marehemu Julieth Majaliwa amesema mara
ya mwisho kuwasiliana na mumewe walikua nyumbani
kwao jijini Dar es salaam ambapo alimuaga anaenda kijijini kwao kuwajulia hali ndugu zake lakini tangu alivyo ondoka hawakuwa tena na mawasiliano nae mpaka waliposikia kwa watu kuwa mume wake amefariki dunia
![]() |
Baadhi ya Familia wa Marehemu wakiangua kilio baada ya kuona mwili wa Marehemu |
Mjomba wa Marehemu aliyefahamika kwa majina ya Mlinga Alpakshad amesema wameamua kumzika marehemu huyo bila kutoa taarifa kwa familia yake kutokana na watoto pamoja na mama yao kumtelekeza wakati alipokuwa anaumwa.
Kwa mujibu wa daktari Msaidizi Mwandamizi George Mkoba kutoka hospitali ya wilaya ya gairo amesema kwa sasa wamechukua baadhi vipimo (SAMPULI) kwa ajili ya kupelekwa kwa mkemia mkuu kwa ajili ya vipimo zaidi kama walivyoagizwa na mahakama.
Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu
Mzee Stanford Gombo amefariki dunia Novemba 11 mwaka huu kijijini hapo baada ya kuugua kwa muda mrefu, huku familia
yake ikiongozwa na Mama na watoto wa nne wakidai kutokuwa na taarifa ya kuugua
kwake mpaka kufariki dunia, hatua iliyopelekea wao kukimbilia mahakamani.
MWISHO
No comments:
Post a Comment