
Kivumbi cha ligi kuu
Tanzania bara kimefika tamati leo katika viwanja 8 tofauti nchini huku
ikishuhudiwa tena timu mbili zikijiunga na timu ya coastal Union tayari kushuka
daraja ambazo ni timu zote kutoka mkoani
Tanga yaani Coastal Union, Mgambo JKT, na African Sports. TANGA kunaniiiiii!!!!
Katika michezo hiyo,
timu ya Simba Sport ikicheza katika uwanja wa nyumbani (Uwanja wa Taifa) imepoteza mchezo wake dhidi ya JKT Ruvu baada
ya kukubali kupigo cha Goli mbili kwa moja, huku magoli ya JKT RUVU yakifungwa
na Abdulhaman Mussa katika dakika ya 2 na 30 huku goli la kufutia machozi la
simba likifungwa na Mussa Mgosi.
Katika uwanja wa Manungu
Mkoani Morogoro, wakata miwa wa Mtibwa Sugar wameibuka na ushindi wa Goli 2 kwa
sifuri dhidi ya wana kimanumanu African Sport ya mkoani Tanga. Magoli hayo ya
wazee wa sukari yamewekwa kimiani na Hussein Javu dk ya 1 na goli la pili
limewekwa kimiani na Jafary Kibaya dk ya 82 ya mchezo huo, mpaka filimbi ya
mwisho Mtibwa Sugar 2 – African Sport 0 hatua inayopelekea timu hiyo kushuka
daraja kuongana na ndugu zao.
Katika uwanja wa chamanzi,
Mbagala wana ramba ramba wa Azam FC
wameradhimishwa sare ya kufungana goli moja kwa moja na JKT Mgambo ya Kibuku Mkoani Tanga, goli la
Azam FC limefunga na Ramadhani Singano huku la mgombo likifungwa kwa njia ya
Penalt, hatua iliyopekea timu hiyo pia kujiunga na coastal, Africani Sport
kushuka daraja.
Katika uwanja wa
Majimaji Mkoani Songea, mabingwa wa ligi
kuu Tanzania Bara Yanga wamelazimishwa sare ya kufungana magoli mawili kwa
mawili na timu ya Majamaji FC ya mkoani humo.
Katika uwanja wa CCM
kirumba mkoani mwanza , wenyeji Toto African wamekubali kichapo cha goli moja
kwa sifuri kutoka kwa timu ya Stand United ya mkoani Shinyanga.
Mkoani Mbeya timu ya
Tanzania Prisons imetoa kipigo kwa timu
ya Coastal Union baada ya kuifunga goli
mbli kwa sifuri na kushika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi kuu Tanzania
Bara.
Mkoani Shinyanga timu
ya kagera sugar imeibuka na ushindi wa goli mbili kwa sifuri dhidi ya timu ya
Mwadui FC.
Kwa matokeo hayo ya
leo timu ya AZAM FC inashika nafasi ya
pili ya msimo wa ligi kuu Tanzania bara, huku SIMBA SPORT KLABU ikishika nafasi
ya Tatu na Timu ya Tanzania Prison ikishika nafasi ya nne nay a tano inashikwa
na wazee wa sukari Mtibwa Sugar.
Kwa upande mwingine
matokeo hayo yamesababisha timu mbili kujiunga na timu ya Coastal Union kushuka
daraja baada ya kupoteza michezo yao, timu hizo ni Mgambo JKT na African Sport.
![]() |
KIKOSI CHA JKT MGAMBO |
Huku mchezaji Amiss Tambwe wa YANGA akiibuka mfungaji bora wa mwaka 2015/2016.
Historia inaonyesha
haikuwahi kutokeanchini timu tatu
zinazotoka sehemu moja kushuka daraja, hatua inayopelekea wadau wa soka
kujiuliza TANGA kunaniii!!!!!!!!!
MWSIHO:
No comments:
Post a Comment