Tuesday, June 21, 2016

JESHI LA POLISI MKOANI MOROGORO LIMEFANIKIWA KUMKAMATA DEREVA WA BASI LA NBS ALIYE SABABISHA AJALI NA KUPELEKEA VIFO VYA WATU 5







Jeshi la polisi mkoani Morogoro limefanikiwa kumkamata dereva Seif shabani wenye umri wa miaka 40 mkazi wa Bacho mkoani Tabora  Dereva wa Basi  lenye namba za Usajili T 909 BXK  mali ya kampuni ya NBS aliye sababisha ajali iliyo pelekea vifo vya watu watano  na majeruhi 27 june 20 mwaka huu katika eneo CHAKWALE wilayani Gairo barabara ya Morogoro-Dodoma.

Kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP-Leonce Rwegasira amesema dereva huyu alitoroka mara baada ya kusababisha ajali hiyo ambapo chanzo cha ajali  kilikua ni mwendokasi uliomfanya  dereva kushindwa kulimudu gari hilo  ambalo liliacha njia na kupinduka.

Kamanda huyo amesema uchunguzi zaidi unaendelea kufanyika kwa kumuohoji mtuhumiwa na pale utakapokamilika utafikwishwa mahakamani kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili.


MWISHO: 

No comments:

Post a Comment