Tuesday, June 21, 2016

JUMLA YA RISASI 853 ZAKUTWA KWENYE DUMU PEMBEZONI WA MTO NGERENGERE.



Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP-Leonce Rwegasira akionyesha risasi hizo kwa Waandishi wa Habari
Jeshi la Polisi  Mkoani Morogoro limefanikiwa kukamata risasi 853 zilizokuwa zikitumika  kwenye silaha aina ya G – 3 zilizokuwa zimehifadhiwa kwenye  dumu na kutelekezwa pembezoni mwa mto wa Ngerengere  maeneo ya Kihonda mkoani humo.

 Kaimu kamanda  wa Polisi Mkoani humo ACP Leonce Rwegasira amesema tukio hilo limetokea Jun 20 mwaka huu katika kata ya Kihonda mkoani humo baada ya askari waliokuwa doria kupewa taarifa na raiawema  na ndipo wapokwenda eneo la tukio wakakuta dumu likiwa limewekwa pembezoni wa mto Ngerengere na kukuta limejaa risasi.


Kaimu wa Kamanda  Rwegasira amesema jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi ili kuweza kubaini wamiliki wa risasi hizo ili kuweza kuwachukulia hatua stahiki za kisheria.


MWISHO:

No comments:

Post a Comment