NA, PETER LAURENCE
![]() |
Gari binafsi aliyokuwa anaitumia mkurugezi wa Halmashauri ya Mkinga |
![]() |
Hapa akijifichwa kupigwa picha na Waandishi wa Habari |
Mtuhumiwa huyo amesomewa
mashtaka mawili mbele ya hakimu Agripina Kimanze chini ya mwendesha mashtaka wa
serikali Sunday Hyera pamoja na Edger Bantulaki, ambapo kosa la kwanza ni
kutishia kuua na la pili ni makosa ya usalama barabarani ambayo yote amekana
kuhusika nayo.
Tukio hilo limetajwa
kutokea October 15 mwaka huu, katika eneo la mkambarani pembezoni kidogo mwa
mji , ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa
akiendesha gari aina Prado ya yenye
namba za usajili T 845 CTJ na aliposimamishwa na askari hao wa usalama barabani
kutokana na kuendesha gari hiyo kwa mwendo kasi, akagoma kutoa ushirikiano kwa
askari aliyemsimamisha na kudai yeye ni mfanyakazi wa serikali.
Baada ya kushindwa kuelewana na askari huyo,
mkurunguzi huyo aliomba kuonana na mkuu wa
kituo katika eneo hilo, hata hivyo wakati akipelekwa na askari mmoja
aliyefahamaika kwa jina moja la Titunda kupitia gari hilo, Mkurungezi huyo
alimtolea bastola askari huyo na kumtaka kushuka kwenye gari na yeye kugeuza na
kuendelea na safari yake, hata hivyo alipofika katika eneo la Mikese, aliweza
kukamatwa na askari waliokuwa wamepewa taarifa juu ta tukio hilo.
Baada ya kukutwa na makosa hayo mtuhumiwa huyo
amefikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo,ikiwemo ya kutishia kuua, kuendesha
gari bila kuwa na bima pamoja na kuendesha kwa mwendo kasi, Makosa ambayo yote
ameyakana.
Mkurugenzi huyo ameachiwa kwa dhamana na kesi yake
imetapangwa kusikilizwa tena Oktoba 31 ya mwaka huu.
MWISHO:
No comments:
Post a Comment