Jumla ya vijana
9100 wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi kutoka katika mikoa ya Dar es
salaam,Lindi, Morogoro,Mtwara na Pwani,wamepatiwa elimuya ufundi stadi, kwa lengo
la kuwakwamua kutoka katika umaskini, huku kipaumbele kikitolewa kwa wenye ulemavu.
| MKuu wa Mkoa wa Morogoro Dr Kebwe Steven Kebwe akikagua moja ya bidhaa ya zilitengenezwa na vijana waliopata elimu ya stadi za kazi katika kijiji cha Mchomwe wilayani Kilombero mkoani humo. |
| Baadhi ya vijana waliyohitimu elimu ya mafunzo ya stadi za kazi kutoka katika kijiji c ha Mchomwe Wilayni Kilombero |
| Vijana walipata elimu ya udereva kutoka chuo cha VETA - Mikumi, wakishangilia kwa furaha mara baada ya kupewa Leseni zao za udereva |
| Vijana Waliopata elimu ya stadi za kazi za ushonaji na Mapambo wakifurahi |
| Kipaji chako ndio ajira yako, mmoja kati ya vijana walipewa elimu na VETA akionyesha ustadi wake katika sekta ya umeme |
Mafunzo hayo
yametolewa na VETA kwa kushirikiana na Plan International, yakiwa na mkakati wa kuwawezesha
vijana 57,300 wanaoishi katika mazingira magumu hasa maeneo ya vijijini,
kupatiwa elimu ya kujiwekea akiba na kuwawezesha kufungua miradi mbalimbali itakayosaidia
kuwainua kiuchumi.
Mafunzo hayo ya ufundi stadi yamelenga kuwafikia
vijana husika maeneo wanayoishi, kwa mifumo ya nadharia na vitendo na pia kwa njia ya uanagenzi, kwa lengo la kuhakikisha ifikapo
mwaka 2020 vijana wengi na wanaoishi katika mazingira magumu wanasaidiwa ili kujikwamua
kiuchumi.
Katika mahafali ya kwanza yalifanyika katika katika kijiji cha mchomwe na ifakara mjini mgeni rasmi alikuwa mkuu wa mkoa wa Morogoro Dr kebwe Steven Kebwe, huku wito ukitolewa kwa mashiriki mengine kuweza kujitokeza na kuwawezesha vijana hasa wale wanaoishi katika mazingira magumu kwa lengo la kuwakwamua,
MWISHO:
No comments:
Post a Comment