MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO AHUKUMIWA MIEZI SITA JELA

Kilombero, Morogoro.
Mahakama
ya Wilaya ya Kilombero imemuhukumu kifungo cha miezi Sita mbunge wa Jimbo
Kilombero mkoani Morogoro kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema Peter Lijualikali wenye miaka (30) mara baada ya kumkuta na hatia
ya kufanya fujo na kusababisha taharuki katika uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti
wa Halmashauri hiyo Machi Mosi mwaka 2016 mwaka wa jana.
Peter
Lijualikali ambaye ni mbunge wa Jimbo la Kilombero pamoja na Stephano
Mgata,wote wawili wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Kilombero, baada ya
kudaiwa kutenda kosa hilo Machi mosi mwaka jana saa nne Asubuhi katika
eneo la Kibaoni katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero,
ambako kulikuwa na uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti wa Halmashauri hiyo.

Washtakiwa
hao kwa pamoja walifanya fujo hizo kinyume na kifungu namba 89, kifungu kidogo
cha kwanza B cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka
2002. Awali
washtakiwa hao kwa pamoja walikana mashtaka na hivyo kufanya kesi hiyo
kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili na upande wa mashtaka ukathibitisha
shtaka hilo bila kuacha shaka.
Hakimu
mkazi wa mahakama ya Wilaya ya Kilombero Timothy Lyon amesema mahakama hiyo
imewatia hatiani kwa kosa hilo na kwa kuwa mshtakiwa wa kwanza Mbunge
Lijualikali ambaye alikuwa na kesi tatu huko nyuma na kutiwa hatiani, basi
anahukumiwa jela miezi sita kutokana na mahakama kuona kuwa ni mzoefu, huku mwenzake ndugu Mgata yeye akihukumiwa kifungo cha miezi sita nje, kutokana na kuoneka ni
mara ya kwanza kuhukumiwa.
Baada ya
kutolewa kwa hukumu hiyo mbunge huyo amepelekwa kwenye gereza la Kilimo la
Idete, ambako ndiko atatumikia kifungo chake cha miezi sita.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment