Tuesday, January 16, 2018

FEDHA BANDIA ZENYE THAMANI YA SHILINGI MIL 40.6 ZAKAMATWA MKOANI MOROGORO

Morogoro
Na, OmaryHussein

Watu watano wanashikiliwa na Polisi mkoani Morogoro, kwa makosa tofauti yakiwemo ya watu  wawili kukutwa na pesa bandia zenye thamani ya zaidi ya shilingi  Milion 40.6 na mabunda 22 ya karatasi zinazotumika  kutengeneza  noti hizo, huku wengine wawili wakikutwa na vipande 4 vya pembe za Ndovu.




Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoani Morogoro SACP Urlich Matei, kukamatwa kwa watuhumiwa wote ni juhudi ziliztotokana  na taarifa kutoka kwa raia wema, ambapo wapo waliotoa taarifa za uwepo wa biashara ya utengenezaji wa fedha bandia katika  Mtaa wa Kihonda  maeneo ya Yespa, nje kidogo ya Manispaa ya Morogoro, na baada ya kufaatilia taarifa hizo, ndipo wakafanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao ambao wamejulikana kwa majina ya Osona Oriko (22yrs) mkazi wa Kihonda pamoja na Yusufu Abdul (12yrs) mkazi pia wa kihonda .



Aidha askari wa jeshi hilo kwa  kushirikiana na maafisa wa wanyama pori  Tarafa ya Mikumi, wamefanikiwa kuwakamata, watu wawili waliojulikana kwa majina ya Shamte Mohamed (22yrs) na Selemani Meya (23yrs) wote wakazi wa ludewa wilayani Kilosa wakiwa na vipande vinne vya pembe za ndovu wakiwa wamevihifadhi katika mfuko wa rambo mweusi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SaCP Matei amesema watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na watafikishiwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

MWISHO.



No comments:

Post a Comment