Tuesday, December 5, 2017

KESI INAYOWAKABILI WABUNGE WA CHADEMA SUZANA KIWANGA NA PETER LIJUALIKALI YAPIGWA KALENDA MPAKA DESEMBA 6 MWAKA HUU

Na, Omary Hussein, Morogoro


Mahakama ya hakimu mkazi Mkoa wa Morogoro, kwa mara nyingine imeshindwa kutoa dhamana kwa Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Peter Lijualikali wa Kilombero pamoja na Suzani Kiwanga wa Mlimba na washtakiwa wengine 34 wa Chama hicho, baada ya kutokea mvutano wa kisheria baina ya upande  wa Mawakili wa Serikali na ule wa utetezi, juu ya kiapo kilichowasilisha na Serikali cha kupinga washtakiwa hao kupatiwa dhamana, hatua iliyopelekea Hakimu Ivan Msaki, kuhairisha tena kesi hiyo hadi Desemba 6, watakapojadili tena kiapo hicho.

Saturday, August 26, 2017

WATUMISHI WATATU WILAYA YA MANYONI WAFUKUZWA KAZI KWA UZEMBE KAZINI

Manyoni, Singida.

Baraza la madiwani katika halmashauri ya wilaya ya Manyoni limewafukuza kazi watumishi watatu wa halmashauri hiyo kwa  makosa tofauti yakiwemo uzembe kazini uliosababisha kifo cha  mjamzito mmoja wakati akijifungua.

Thursday, August 24, 2017

WATU SABA WAMEFARIKI DUNIA BAADA YA BUS KUPINDUKA KATIKA MILIMA YA NDOLOLO


NA, PETER LAURENCE
MOROGORO
24/08/2017


Watu Saba wamefariki Dunia  wengine 38 wakijeruhiwa wilayani Ulanga Mkoani Morogoro mara baada ya Bus walilokuwa wakisafiria   kupinduka katika Milima ya Ndololo, huku miili ya watu hao waliofariki dunia ikihifadhiwa katika  chumba cha mahiti cha hospitali ya wilaya ya Mahenge.



WATU WATATU WAFARIKI DUNIA BAADA YA GARI AINA YA HAICE KUGONGA TRENI MKOANI MOROGORO


NA, FARID SAIDY
MOROGORO
24/08/2017


Watu watatu wamefariki Dunia huku wengine 29 wakijeruhiwa, baada ya daladala waliyokuwa wakisafiria kugonga Treni ya abiria iliyokuwa inatokea bara kwenda Dar es salam katika eneo la Tanesco Manispaa ya Morogoro, huku idadi hiyo ya Majeruhi wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa Shule  za Sekondari za  Tushikamane na Mji Mpya.

Wednesday, January 11, 2017

MBUNGE WA JIMBO LA KILOMBERO AHUKUMIWA MIEZI SITA JELA

Kilombero, Morogoro.


Mahakama ya Wilaya ya Kilombero imemuhukumu kifungo cha miezi Sita mbunge wa Jimbo Kilombero mkoani Morogoro kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema Peter Lijualikali wenye miaka (30) mara baada ya kumkuta na hatia ya kufanya fujo na kusababisha taharuki katika uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Machi Mosi mwaka 2016 mwaka wa jana.


Monday, October 17, 2016

DED WA MKINGA APANDISHWA KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUMTISHIA KUMUUA NA BASTOLA ASKARI WA USALAMA BARABARANI


NA, PETER LAURENCE
Bastola ya Mkurugenzi Huyo iliyoitumia kumtishia kumuua askari wa usalama Barabarani


Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro limemfikisha mahakamani Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mkinga mkoani Tanga Emmanuel Mkumbo mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam, kwa tuhuma za kumtishia  kumuua kwa  bastola askari wa usalama barabarani, wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi pamoja na kuvunja sheria za usalama barabarani.

WAZIRI LUKUVI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA OFISI YA MASJALA YA ARDHI MANISPAA YA MOROGORO

Na, Omary Hussein, Morogoro.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,

Waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi William Lukuvi amefanya ziara ya kushtukiza katika ofisi ya Masjala ya Ardhi Manispaa ya Morogoro na kukuta hati zaidi ya 100 ambazo zimekamilika lakini bado hazijatolewa kwa wahusika huku Maofisa wa Ardhi katika ofisi hiyo wakishindwa kutoa sababu za msingi za kuchelewesha kutolewa kwa hati hizo.